|
Post by abtitchaz on Jul 30, 2008 3:02:28 GMT 3
Utamu wa Tunda la kuiba - Kwanini?
Nabisha hodi watani, mjuao Kiswahili, Nimetingwa mawazoni, sasa nauliza swali, Jibu niandikieni, moyo wangu ukubali, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Ni tunda naulizia, lile lililonawiri, Si langu nawaambia, la kwake bwana Bushiri, Miye nimetamania, njama nikatafakuri, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Mwenyewe yuko kazini, shamba liliko ni mbali, Zamu yake ni jioni, asubuhi yangu mali, Nalila kiulani, pasipo ya mushkeli, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Tunda silili kwa pupa, na silili kibahili, Siling’ati kwa kuepa, kama vile mbilikili, Mbegu yake sitotupa, namung’unya kimahili, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Utamu wake adimu, unaizidi asali Tunda hili siyo ndimu, na wala siyo figili, Ninaling’ata kwa zamu, unasisimka mwili, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Siogopi kuja bambwa, na yeye bwana Bushiri, Ni fumbo lilifumbwa, tunda sitalighairi, Hata akileta Mbwa, nalifunguia safari, Kula tunda kwa kuiba, kwa nini huko kutamu?
Beti zangu nazifunga, jibu lenu nasubiri, Mlo mabingwa kutunga, mnijibu kishairi, Na hata mso malenga, nijibuni bila shari, Kula tunda kwa kuiba, kwanini huko kutamu?
Na. M.M.Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
|
|
|
Post by a.k.a on Aug 1, 2008 11:40:11 GMT 3
abtitchaz kwanza niambie kama ninawaza sawia....hapa tunda la simamia "mke wa mtu" ?
|
|
|
Post by abtitchaz on Aug 4, 2008 16:59:10 GMT 3
abtitchaz kwanza niambie kama ninawaza sawia....hapa tunda la simamia "mke wa mtu" ? mmmhhh!!!?...ni mojawapo ya tunda.Hujakosea.
|
|
|
Post by a.k.a on Aug 5, 2008 11:32:10 GMT 3
sawa sawa,naona sijakisahau kiswahili changu...ebu kidogo uchambua hilo shairi.
|
|
|
Post by nora on Aug 9, 2008 7:44:30 GMT 3
kama tunda ni manzi....basi the poem is a about a stolen chick? as in the sweeteness of a stolen chick?
|
|